HOME.


KILIMO BORA CHA PILIPILI MBUZI

UTANGULIZI
Pilipili mbuzi ni zao ambalo linaweza kulimwa kibiashara na kumpatia faida nzuri mkulima. Zao hili huitaji mwanga wa kutosha wa jua (ingalau kiasi cha masaa 6 kwa siku) 


Pilipili hustawi vizuri zaidi kwenye udongo wenye mbolea ya asili, undongo wenye unyevu nyevu ila usiwe wenye kutuamisha maji. Pilipili mbuzi huitaji udongo wenye pH 6.0 hadi 6.8, Ikiwa pH ni chini ya 6.0 ongezea madini chokaa kwenye udongo; Na ikiwa pH ya udongo imefika 8 onana na wataalam wa kilimo wakushauri namna ya kuipunguza.

 

KUANDAA MICHE
Mbegu za pilipili huoteshwa miche kwenye kitalu kabla ya kwenda kupandikizwa shambani. Pandikiza mbegu kwenye kitalu week 7 hadi 10 kabla ya kipindi ambacho umepanga kupandikiza miche shambani. Panda mbegu tatu tatu kwenye kila kishimo na chagua mbili zilizo chipua vizuri kwa ajili ya kuhamishi shambani.

 

KUHAMISHA MICHE SHAMBANI
Hamisha miche shambani ikiwa imetengeneza majani 8, ingawa kuhamisha ikiwa na majani machache au mengi zaid haitapelekea shida yoyote.

 

MUHIMU...Unashauriwa kuhamisha miche shambani kwa kuzingatia mambo yafuatayo.
Siku ya kwanza kwa lisaa limoja weka miche kivulini au mahali ambapo kuna kizuizi jua la moja kwa moja lisiifikie miche. Kadri siku zinavyo kwenda ruhusu miche kupata mwanga wa jua zaidi.
Chimba mashimo marefu kuzidi urefu wa mizizi ya miche kisha changanya vyema udongo na mbolea ya Ngo’ombe. Muda mzuri wa kuhamisha miche yako shambani ni jioni au kipindi ambacho jua limefifia kuepuka miche kukauka.


Changanya sulphur (Tembe 2) kwenye maji na kumwagilia na rudia mchanganyo huu kila baada ya week mbili. Sulphur husaidia kuuwa fungus, inauwa bacteria wasio faa, kuzuia magonjwa pia huasaidi mizizi kusambaa na kukua kwa haraka na kupata virutubisho.


Mwagilia miche maji ya kutosha baada ya kuihamishia shambani hiyo husaidia kupunguza stress za mmea unapobadilishiwa mazingira. Tumia mbolea ya Miracle Gro kila baada ya week mbili.

 

MAHITAJI YA MMEA
Pilipili ni zao lenye kuhitaji zaidi unyevu unyevu shambani ila maji yasiwe yenye ktuama. Kipindi ambacho maua yametoka na vitunda vya pilipili vimeanza kujitokeza, udongo ukiwa mkavu sana hauna unyevu wa kutosha hupelekea maua kudondoka. Epuka umwagiliaji ulio zidi mahitaji au ulio chini ya mahitaji. Unaweza kutandaza nyasi kwaajili ya kusaidia kuhifadhi unyevu shambani. Mmea huanza kutoa maua mapema baada ya kutengeneza matawi, Mau ya mmea hua na set iliyo kamilika (jike na dume) hivyo kuwa na sifa ya kuweza kujichavusha yenyewe. Upepo, wadudu au kwakutumia mkono husaidia kuongeza uchavushaji.

 

KUPALILIA
Pilipili zi zao ambalo halina mizizi mirefu sana, hivyo basi mkulima anapaswa kuzingatia hilo na kuongeza umakini wakati wa kupalilia kuepuka kukata mizizi.

 

MAGONJWA
Pilipili inaweza kushambuliwa na magonjwa yafuatayo, blossom end rot, anthracnose, tobacco mosaic virus, bacterial spot, and mildew. Namna ya kulinda mimea yako dhidi ya magonjwa hayo weka shamba lako katika hali ya usafi na ondoa magugu shambani kuondoa sehemu za mazalia ya wadudu. Ondoa mimea iliyo athiriwa kabla ugonjwa haujasambaa shambani.

MAVUNO
Pilipili huwa tayari kwa kuvunwa siku 60 hadi 95 kutegemea na aina ya mbegu uliyotumia. Chuma kwa uangalifu bila kung’oa mmea ili uendelee kuzalisha. Muvuno yanaweza kudumu kwa muda wa mwezi 1 hadi 3.

 

USALAMA WAKATI WA UVUNAJI
Pilipili huwa na kemikali iitwayo capsaicinoids ambayo inaweza
kukuwasha kwenye ngozi au kwenye macho ikiwa utajigusa. Vaa gloves wakati wa kuvuna na kuwa mwangalifu usijiguse kwenye macho.

 

SOKO
Fursa
Pilipili ni zao ambalo halina mbadala wake au (substitute) hivyo kufanya mahitaji yake kuwa ni ya muda wote bila kutetereka.

 

Changamoto
Muda ambao wakulima wengi wanakuwa wamezizalisha zaidi huathiri sana soko la pilipili kwa maana hata bei ikishushwa sana haiwezi kushawishi watumiaji kutumia pilipili nyingi zaidi.

Kuepuka changamoto hiyo wakulima wanashauriwa kupunguza huduma shambani hadi pale soko litakapo tengemaa vizuri.

 

MBINU ZA MAFANIKIO KWENYE KILIMO

1. ZALISHA KWA WINGI
Uzalishaji mkubwa husaidia sana kupunguza gharama ambazo haziepukiki yani (Fixed Cost). Ukizalisha kwa wingi kwa gharama ndogo utaweza pia uza bidhaa zako kwa bei ndogo na bado utapata faida nzuri na kujihakikishia soko la uhakika kwa bidhaa zako.

 

2. TAFUTA MASOKO YA BIDHAA KABLA YA KUANZA UZALISHAJI
Mkulima mwenye mafanikio ni lazima pia awe mfanya biashara mzuri ukiachilia mbali kuwa mzalishaji mzuri. Mkulima ni vyema kutengeneza channels mapema kupata wateja wa mazao yako. Ukizalisha kwa wingi kwa gharama ndogo itakusaidia sana kwenye kupata masoko utakwa na ushawishi zaidi kwa wateja. Tengeneza wateja na wateja watakutengenezea biashara.

Mteja anataka vitu vitatu vya msingi.

-Unafuu wa bei
-Ubora wa zao
-Upatikanaji wa uhakika wa bidhaa

Ukijihakikishia hivyo vitu vitatu hapo juu hapana shaka utakuwa umejihakikishia soko la uhakika

3. USILIME KWA KUFUATA MSIMU
Unapolima kwa kufuata msimu, mtajikuta wakulima wengi mmezalisha zao fulani kwa wiiingi kwa kipindi kimoja hivyo kupelekea upatikanaji wa zao hilo kuwa mkubwa kuliko inavyo hitajika kwenye masoko, jambo hili hupelekea mazao kuuzwa kwa bei ndogo na kupelekea wakulima kukosa faida ya kutosha au hata kupata hasara muda mwingine.

Unapolima kwa kutofata msimu mkulima utaweza kuzalisha zao/mazao kipindi ambacho wengine hawazalishi hivyo mahitaji yatakuwa makubwa na upatikanaji wa zao hilo utakuwa ni mdogo hivyo mkulima ataweza kupanga bei nzuri kwa mazao yake.


(FANYA KILIMO CHA UMWAGILIAJI)

4. USIFANYE KILIMO KWA MAZOEA
-Tumia wataalamu wa kilimo
-Tumia njia za kisasa za kilimo
-Fanya utafiti wa ardhi dhidi ya zao unalotaka kufanya (Tumia wataalamu)
-Fanya kilimo cha umwagiliaji uweze kuzalisha kipindi ambacho wengine hawawezi kuzalisha ili uuze mazao yako kwa bei nzuri zaidi.

 

FAIDA ZA KUTUMIA PILIPILI
1. Pilipili inasaidia sana kusawazisha sukari kwenye damu

2. Ulaji wa pilipili kunaweza kunawasaidia sana watu wanene (overweight) au wanao ugua ugonjwa wa kisukari. Hii ni kwa mujibu wa timu ya watafiti katika Chuo Kikuu cha Tasmania, utafiti iliyochapishwa katika American Journal of Clinical Nutrition, mwezi Julai 2006.

3. Utafiti huo pia umeonyesha kwamba kawaida ya kula Pilipili kunaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti na kusawazisha insulini kwa 60%. baada ya kula chakula.

4. Pilipili husaidia kupunguza maumizi na uvimbe kwenye tezi na vilevile huwasaidia wagonjwa wa rheumatoid na arthritis kupata nafuu. Vile vile husaidia kuondoa mkusanyiko wa damu sehemu moja ya mwili

5. Pilipili usaidia kufungua kwa haraka na kwa ufanisi pua zilizoziba kwa mafua, kuruhusu kupumua kwa urahisi zaidi!

6. Pilipili pia husaidia kupunguza upatikanaji wa saratani ya kwenye tumbo (Stomach Cancer)

7. Pilipili usaidia kuongezeka kwa kiwango cha metabolic, ambayo husaidia kuchoma mafuta, ulaji wa pilipili kunaweza kuinua kiwango na metabolic yako hadi 23% ndani ya masaa 3.

8. Kula pilipili usaidia kupunguza cholesterol, na kupunguza kiasi cha fibrin katika damu


NOTE; Kula kupita kiasi ni hatari pia kwa afya yako

 

KWA MAONI NYONGEZA AU USHAURI TUNAKARIBISHA MAWAZO YA WADAU WENGINE










 

 

 

KILIMO CHA PILIPILI MBUZI (PILIPILI UGANDA)

MBEGU NA JINSI YA KUSIA/KUMWAGA.

Tafuta mbegu bora iliyoandaliwa kitaalamu kwa Tz unaweza pata mbegu bora ya pilipili mbuzi kutoka Kampuni ya ..... AYEGRO Group Ltd.Mbegu 100g zinatosha kupanda ekari moja.

Andaa kitaru chako vizuri chenye ukubwa wa mita moja kwa sita ((1 x 6) m),Ili hewa iweze kuzunguka vizuri kwenye udongo unashauriwa kutengeneza kitaru mbinuko.Kama una mbolea aina ya samadi iliyooza vizuri (Well decomposed) changanya debe 3 kwenye kitaru cha mita moja kwa sita.Hakikisha unachanganya vizuri udongo na samadi hadi ushindwe kutofautisha kati ya samadi na udongo,baada ya kuchanganya samadi na udongo sasa sawazisha vizuri,hakikisha hakuna mabongemabonge.

Kama huna mbolea ya samadi tumia DAP baada kuanda kitaru chako rushia DAP kiasi cha 180g kwa kitaru cha mita moja kwa sita au kwa lugha nyingine ni 30g kwa kila square mita moja

Baada ya kuweka mbolea tengeneza mistari inayopishana kwa umbali wa sentimita 4 na baada ya hapo sia/mwaga mbegu zako kwenye hiyo mistari NB:Usibananishe mbegu.

Baada ya kuweka mbegu kwenye hiyo mistari fukia vizuri kwa kutumia udongo laini na kisha tafuta majani makavu na tandika kitaru chako vizuri na baada ya hapo mwagilia maji ya kutosha kwa kutumia Keni ya kumwagilia.

Mbegu zitaota baada ya siku 7-10 na baada ya kuota toa majani na kama ni masika tengeneza kichanja na tandika juu ya kichanja,kama ni kiangazi unaweza kuacha kuweka kichanja.

Siku mbili baada ya mbegu kuota mwagilia maji ya kutosha na kisha pulizia Actara au dawa yoyote yenye kiambato sawa na Actara.Pulizia dawa nyingi mpaka udongo ulowane zaidi(Drenching).Pima Actara 8g/20L.

Siku 4 baada ya mbegu kuota pulizia Ridomil gold au ....pima 50g/20L. Baada ya siku 14 tangia upulizie Actara rudia kupulizia tena na vivyohivyo kwa Ridomil gold na pia rushia Yaramila winner kidogo.

Miche ya pilipili mbuzi hukaa kwenye kitaru siku 30-35 na baada ya hapo unahamishia shambani.

UPANDAJI.

Andaa shamba lako vizuri,muonekano wa shamba utategemea njia unayotumia kumwagilia.Panda kwa kuzingatia nafasi. Kutoka mmea na mmea iwe kati ya 30-60 cm na mstari na mstari iwe kati ya 70-100 cm (Kulingana na aina ya mbegu).Pandia DAP 5g /mmea.Hakikisha mbolea haigusani na mizizi au Panda miche bila mbolea mwagilia maji na kisha tengeneza starter solutions.NB:Chukuwa kilo 3 za DAP weka kwenye maji lita 200 na kisha kologa mpaka mbolea yote iyeyuke na kisha chota kwa kutumia kikombe cha chai kidogo na mwagilia miche yako aliyopanda siku hiyo,hakikisha maji yenye mbolea hayagusi majani ya miche yako...mwagilia chini kwenye udongo tu sio majani.

 

MBOLEA.

Siku 10 Baada ya kupanda sasa endelea kukuzia mbolea,wakati huu tumia Yaramila winner 5-10g kwa mche.NB:Usitupie juu..hakikisha mbolea unaifukia kuzunguka mmea na usiweke karibu sana na mmea,weka 4-6 cm kutoka kwenye mmea.

Na kila baada ya siku 21 weka mbolea aina ya Yaramila winner au NPK Isipokuwa wakati maua yameanza weka Yaramila nitrabo au CAN 10g /plant,na baada ya hapo utaendelea na Y-winner mpaka mwisho wa mavuno.

 

WADUDU
Pilipili mbuzi hushambuliwa na ;
A) Wadudu mafuta ( Aphids)

Kuwadhibiti.

Tumia Actara 8g/20L.
Au tumia wadudu wanaokula wadudu mafuta,mfano special beetles.

B) Crickets
Hawa wadudu hukaa aridhini karibu na mmea na usiku hutoka walipo jificha na kukata miche michanga.

Kawadhibiti.
Unapo andaa shamba andaa vizur ili nyumba zao zife na kuwaacha katka halu ya hatari ya kuliwa na ndege na wadudu wengine ,kama ni miche na iko kwenye tray...basi weka hizo tray juu ya kichanja.

C) Beetle.
Tuma Karate 40cm/20L.

D) Utitiri

Dawa:Tumia Dynamec au yoyote yenye Abamectin.

E) Nematodes na nk.
Tumia solvigo.

MAGONJWA.
1) Fusarium wilt (Mnyauko)
Njinsi ya kuepuka.

.Tandika shamba lako na majani makavu ili kupunguza joto.
.Ng'oa mimea yote iliyougua na choma moto mabaki.
.Epuka kusambaza ugonjwa kwa kusafisha vizur vifaa vya shamba na chini ya miguu uingiapo shambani.
.Jitahidi mimea iwe na afya nzuri kwa kuweka mbolea na maji ya kutosha.
.Pulizia dawa ya fangas kama vile ortiva.

2) Southern blight ( Sclerotium wilt)
Huu ungonjwa utaona kwenye shina china panaota fangasi weupeweupe (Whitish fungal growth on the stems of infected plant) .Majani ya chini huweza kunyauka,Huu ungonjwa hutokea muda mfupi kipindi cha joto kali.

Kuepuka/Kuzuia.
.Wakati wa kulima ..lima hadi chini sana ili hao fangasi waende chini sana ambapo mizizi haifiki.
.Mimea iliyoshambuliwa...Ing'oe yote na choma moto lakini chomea nje ya eneo la shamba.
.Pulizia Ortiva.

3) Anthracnose.

Huu ni ugonjwa wa kawaida kwenye pilipili mbuzi na huu ugonjwa huweza kukaa ardhini muda mrefu.Dalili zake utaona matunda kama kuna sehemu zinakuwa nyeusi na panajaa majimaji ...dalili hii huenea sehemu kubwa ya tunda na baadaye tunda huoza.

Kuepuka.
Kuepuka ugonjwa kujirudia musimu na musimu..Baada ya kuvuna choma mabaki yote.

.Shamba ambalo ulilima pilipili usirudie kulima pilipili mfululizo zaidi ya mara mbili...badilisha zao kwa kupanda zao ambalo sio jamii moja na pilipili mbuzi (Do crop rotation)
.Pia huu ugonjwa huweza kupitia mbegu...kwa hiyo mkulima lazima achukue mbegu kutoka kwa wakala aliyeidhinishwa na mwaminifu...mbegu hazitakiwi kutengenezwa kutoka kwenye mimea iliyoathirika na ugonjwa.

4) Bacteria.
Madoamadoa ya bacteria kwenye matunda....huweza kutokea na kusambaa haraka wakati wa joto kali na unyevu kwenye udongo.Pia huu ugonjwa huweza kuenea kupitia mbegu.

Dalili zake utaona madoamadoa ya kama brown chini ya majini na pia kwenye matunda.

Kuepuka.

.Usitengeneze mbegu kutoka kwa mimea iliyoathirika na huu ugonjwa.Nunua kutoka kwa wakala.
.Pulizia dawa yoyote copper.

5) Virusi.
Kuna aina nyingi ya virusi ambao hushambulia pilipili mbuzi.
Dalili zake ni majani kuwe ba njano na kujikunja .

Kuepuka.
.Nunua mbegu bora
.Pulizia dawa za wadudu kuanzia kwenye kitaru na kuendelea.Wadudu wanaosababisha virus sanasana na wadudu mafuta (Aphids) kwa hiyo akikisha muda wote shambani hakuna hao wadudu kwa kupulizia Actara.

NB:Pamoja na maelezo yote hapo juu.Usikae zaid ya siku 14 bila kupiga dawa ya wadudu na ukungu/fangasi hata kama hakuna ugonjwa wala wadudu.

Mavuno.

Utaanza kuvuna baada ya siku 90 tangia uhamishie miche shambani na utaendelea kuvuna kwa muda wa miezi 6-12 kulingana na matunzo yako.

Kila wiki unavuna na kila ukivuna kwa ekari moja hutoa gunia 10-20 kulingana na huduma yako pia.

Soko na bei.
Soko la pilipili mbuzi Tz ni kubwa sana japo kuna muda zinashuka bei lakini bado mkulima anapata faida.

Bei ikipanda sana huwa Debe ni Tsh 30 000-60 000.Hii mara nyingi hutokea miezi ya 1-7 na bei ikishuka huwa Debe ni Tsh 10 000-25 000 .Hii mara nyingi hutokea miezi ya 7-12.

Changamoto
Usipozingatia maelekezo ya wataalam au wakulima wazoefu unaweza ukapata hasara kubwa.

By Agronomist Peter

Kwa kutoa order ya mbegu bora ya pilipili mbuzi/Pilipili Uganda, piga simu kwa Mkurugenzi mkuu wa AYEGRO Group Ltd Tz, kwa simu no.
+255623642293.

Top of Form

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

SOKO LA PILIPILI MBUZI

 

 

Na Hawa Mohamed na Tulinkisa Ndelwa  


 

      

Kijiji cha Luganga katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini kina wakulima wengi wa pilipili, Wakulima hao wanakabiliwa na changamoto kadhaa katika kuwa na soko la uhakika la zao la pilipili mbuzi. 

 

Changamoto moja inatokana na ulimbukeni wa kukurupuka kulima pilipili kwa wingi kwa kutarajia kuwa bei nzuri ya msimu uliopita ndiyo itakuwa bei ya msimu unaofuata. Wakulima hao wamejikuta wakiingia katika mkumbo wa kuchangamkia kilimo cha pilipili mbuzi kutokana na msimu mzuri uliopita.Wakulima wengi hubabaika na hulima wakiangalia zao lenye bei nzuri na pindi bei inapoporomoka na kuwatia hasara wakulima hao huamua kuachana na pilipili mbuzi kabisa.

 


Mbali na hasara inayoweza kumkuta mkulima kwa kulima kwa wingi kwa matarajio ya bei kubwa na hivyo kuchangia mavuno kufurika na kuharibu bei, wakulima pia hukabiliwa na kutofahamu yaliko masoko ya bidhaa yao na hivyo kulazimika kutegemea wafanyabiashara wa kati – madalali. Madalali hao hununua pilipili mbuzi kwa bei ndogo kutoka kwa wakulima na kisha kuiuza kwa wafanyabiashara wengine kwa bei kubwa.

 

Mkulima YOHANES JUMANNE katika kijiji cha luganga, aliongea na IBER akasema alijiikuta anashindwa kung'ang'ania bei ambayo ni kinyume na matakwa ya madalili. Aisema moja ya vitu vinavyomfanya akose nguvu ya kudai bei bora zaidi ni kwamba soko linakuwa limefurika kiasi cha kuwafanya wakulima wengine kuachana kabisa na kilimo cha pilipili mbuzi. Aliongezea na kusema ufumbuzi unaweza kuwa eneo ambalo linatambulika wazi kuwa ni soko la pilipili mbuzi.

 

Kuwepo kwa soko la kudumu ni kitu ambacho kinaweza kumsaidia mkulima kupata kipato zaidi. Bei ya mazao inakuwa ni yakueleweka kwa kuwa hakutakuwa na madalali, wakulima watapata fursa ya kujiendesha wenyewe pia inaongeza ujuzi na maarifa juu ya soko na biashara kutokana na uwepo wa wataalamu juu ya masoko.

 

FIKIRA KISSIMBA ni Katibu Tawala Msaidizi, Uchumi na Uzalishaji, mkoa wa Iringa. Yeye alisema wakulima wasioweza kupata wateja wa mazao yao kwa haraka wanapaswa kuwa na eneo ambako ndio pekee pauziwe mazao yao.


 

 

Mindombinu ya uzalishaji, usafirishaji, uhifadhi na usindikaji ni muhimu katika kuimarisha uhakika wa masoko ya mazao ya kilimo. Japo bado kuna changamoto ya uelewa mdogo kwa wakulima. Licha ya kuwepo vikundi mbalimbali vya wakulima, bado ni wakulima hawajajiunga kwenye vikundi hivyo huathiri utendaji wa wataalamu wa kilimo. Jambo hili pia huchangia kukosekana kwa taarifa muhimu ikiwemo namna ya kukabiliana na changamoto zinazowakumba wakulima. Lakini wakulima wanapojiunga katika vikundi huku kila mmoja akiwa na mawazo tofauti na mwenzake, hupelekea kushindwa kuafikiana. Kumbe, kama anavyoeleza Katibu Tawala Fikira Kissimba, vikundi vyenye maafikiano vinaweza kusaidiwa mbinu mbalimbali zinaoweza kukabiliana na kufurika kwa soko, ikiwa ni pamoja na usindikaji wa mavuno ya ziada.

 

Faida ya wakulima kuwa kwenye vikundi inakwenda mbali zaidi kuliko kuwapa nguvu kwenye soko. Kuwa pamoja kunaisaidia serikali au wadau wengine kuwafikia wakulima kwa urahisi ili kutoa usaidizi wa kitaalamu wa kuboresha zao lao.

 

Nae Afisa Kilimo kata ya Ilolo Mpya, BWANA PETER SHAYO, alisema serikali inaweza kuwa na usaidizi mzuri kwa wakulima iwapo watalima pamoja katika vikundi. Anasema hilo linaweza kusaidia hata kwenye upatikanaji wa madawa.

 

Matokeo ya piilipili  kufurika katika soko hupelekea kuingia kwa madalali ambao wanawanyonya wakulima kwa kuwabana kwenye bei ya shambani.

 

Nini kifanyike?

Kutengwa  maeneo mahususi kwa uuzaji na ununuaji wa pilipili kutawapa wakulima uhakika wa soko na kujikinga na madalali wanaowanyonya. Nguvu ya wakulima pia inaongezeka kwa kuwa kwenye vikundi na hivyo kutohitaji madalali, kwa kuwa pia wanaweza kusaidiwa mikopo, madawa na ushauri na wadau wasiowanyonya. Na pia wakulima kupatiwa ustadi wa kusindika mavuno ya ziada.

 
Mzigo wa kuboresha soko kwa zao lao hilo, kwa sehemu kubwa limo mikononi mwa wakulima wenyewe. Wawe na ushirikiano ili wawe na nguvu na pia waweze kupata usaidizi