Kabla ya kusindika vitunguu saumu
ni muhimu kuhakikisha kuwa vitunguu vinavyosindikwa vimekomaa vizuri na vipo
kwenye kiwango cha ubora na havijaoza.
DALILI
ZA VITUNGUU SAUMU VILIVYOKOMAA
1.
Vitunguu
saumu huwa tayari kuvunwa katika kipindi cha miezi mitatu hadi mitano tangu
kusia Mbegu
2.
Vitunguu
saumu vilivyokomaa huonyesha majani kunyauka na kubadilika rangi na kuwa ya
manjano hadi kahawia.
3.
Shingo
ya vitunguu saumu hulegea na majani yake huanguka.
BIDHAA
ZITOKANAZO NA KUSINDIKA VITUNGUU SAUMU
Kitunguu saumu huweza kusindikwa ili
kuongeza thamani kwa kuzalisha bidhaa ambazo ni pesti pamoja na unga.
KUSINDIKA KITUNGUU SAUMU ILI KUPATA
PESTI (LAHAMU)
Kuna njia mbalimbali za
kutengeneza lahamu ya vitunguu saumu, lahamu nyingine huchanganywa na viungo, na
nyingine hutumia vitunguu saumu ambavyo vimepikwa kidogo. Vifaa kwa ajili ya
kusindika ni pamoja na kisu kikali kisichoshika kutu, meza safi yenye kufunikwa
na bati la aluminiamu, chupa zenye mifuniko imara, mashine ndogo ya kusaga
vitunguu saumu, jiko, sufuria, lebo, lakiri na mizani. Malighafi ni pamoja na
vitunguu saumu, maji safi, chumvi, siki au sodiamu benzoate na mafuta ya maji.
JINSI
YA KUSINDIKA
1.
Chagua
vitunguu saumu ambavyo havina ukungu na mikwaruzo na ondoa magamba kwa kutumia kisu.
2.
Ondoa
vikonyo vyote na menya kisha osha kwa maji safi na salama.
3.
Weka
vitunguu saumu safi vilivyomenywa kwenye sufuria ya maji safi yanayochemka kwa muda
wa dakika moja.
4.
Ondoa
kwenye maji na saga kwa kutumia mashine kisha pima uzito wa pesti.
5.
Ongeza
chumvi asilimia 5, yaani gramu 50 kwa kila kilo moja ya pesti.
6.
Ongeza
ndimu au siki maalumu (balsamic
vinegar) gramu 30 kwa kila kilo moja ya
pesti.
7.
Ongeza mafuta ya maji kiasi cha gramu 30 kwa
kila kilo moja ya pesti. Hii husaidia vitunguu kuhifadhiwa kwa muda mrefu.
8.
Koroga
mchanganyiko hadi uwiane na fungasha kwenye chupa safi zilizochemshwa.
9.
Panga
chupa kwenye sufuria kisha weka maji hadi yafikie nusu kimo cha chupa hizo na
chemsha kwenye moto wa kadiri kwa muda wa dakika 25 hadi 30.
10. Ipua, acha zipoe kisha weka lebo na
lakiri.
11. Hifadhi sehemu yenye ubaridi, kavu
na yenye mwanga uliofifia.
12. Vitunguu saumu vilivyosindikwa vizuri
huweza kuhifadhiwa kwa zaidi ya miezi sita katika hali ya kawaida bila
kuharibika.
MATUMIZI YA PESTI YA VITUNGUU SAUMU
Pesti ya vitunguu saumu hutumika
kama kiungo katika vyakula mbalimbali, dawa ya kutuliza magonjwa na kuzuia
magonjwa mengine.
KUSINDIKA VITUNGUU SAUMU KUPATA UNGA
Vifaa vinavyohitajika ni pamoja na
kaushio bora, mashine ya kusaga, kisu kisichoshika kutu, chekeche, mabeseni na
chupa za kuweka viungo. Maligafi ni vitunguu safi visivyokuwa na ukungu.
JINSI YA KUTENGENEZA
1.
Chagua
vitunguu saumu ambavyo havina ukungu wala magonjwa na menya kwa kutumia kisu kisichoshika
kutu.
2.
Osha
kwa maji safi na salama kisha katakata vipande vidogovisivyozidi unene wa
milimita 2.
3.
Kausha
kwa kutumia kaushio au kichanja bora kisha saga kwa kutumia mashine ili kupata
unga.
4.
Chekecha
unga huo ili kupata unga laini na fungasha kwenye chupa safi zilizochemshwa na funga
kwa mifuniko.
5.
Weka
lakiri na lebo kisha hifadhi sehemu iliyo baridi, kavu na yenye mwanga hafifu.
MATUMIZI YA UNGA WA VITUNGUU SAUMU
Hutumika kama kiungo katika
vyakula mbalimbali kama ambavyo kitunguu saumu kibichi inavyotwangwa na kutumiwa.
SAID NGUZO
MANGO
PICKLE ZINAZOZALISHWA NA
MWANDISHI WA MAKALA HII
MALI
GHAFI:
1.
Embe
2.
Sukari
3.
Pilipili nyekundu
4.
Haladali
5.
Uwatu
6.
Siki/Vinegar
7.
Mafuta ya Alizeti/Mafuta yasiyoganda
VIFAA
VITAKAVYOTUMIKA:
1.
Ndoo ya plastiki
2.
Sufuria kubwa
3.
Dishi la plastiki
4.
Sufuria ndogo
5.
Mwiko kwa ajili ya
kukorogea
6.
Brush
7.
Visu visivyoshika kutu
8.
Jiko
9.
Meza yenye bati la
aluminium
10.
Mzani
11.
Kinu au blender
HATUA
ZA UVUMBIKAJI:
1.
Osha embe kwa maji safi yaliyochemshwa na
kupoa
2.
Katakata embe bila kumenya vipande vidogo
kwa kisu kisichoshika kutu
3.
Weka chumvi kulingana na kiasi cha embe
ulichopata, mfano:
Kilo 20 za embe changanya na kilo
tatu za chumvi. (changanya vizuri)
4.
Weka kwenye jaba au ndoo na funga vizuri,
Hakikisha hewa haiingii halafu hifadhi sehemu salama
5.
Acha kwa wiki nne mpaka sita, lakini kila
wiki tazama chumvi kama badi ni ya kutosha. Kama haitohi basi ongeza kilo moja
kwenye kilo kumi.
ZINGATIA:
Embe hii
iliyosindikwa hukaa kwa muda wa miaka mitatu mpaka mitano.
UTENGENEZAJI WA ACHALI SASA BAADA YA
UVUMBIKAJI WA EMBE
1.
Osha embe mara tatu kwa maji safi
yaliyochemshwa na kupoa ili kuondoa chumvi
2.
Weka kwenye chujio kwa masaa 24 (siku
nzima) ili kuchuja maji.
3.
Pima uzito ili uweze kujua kipimo ikusaidie
katika uchanganyaji na malighafi nyingine
KUCHANGANYA:
1.
Ndoo ndogo (lita kumi)
a.
Uwatu uliokaangwa na kusagwa vijiko sita
vya chakula
b.
Haladali iliyokaangwa na kusagwa vijiko
vitatu vya chakula
c.
Sukari vijiko vitatu vya chakula
d.
Pilipili nyekundu robo kilo
2.
Changanya na koroga kupata mchanganyiko
mzuri
3.
Weka siki chupa tatu/lita tatu
4.
Weka mafuta ya kula kikombe kimoja kile
kidogo cha ndani cha chupa ya chai.
5.
Funika kwa dakika kumi
6.
Funua na koroga kupata mchanganyiko.
7.
Weka kwenye vifungashio, ongeza mafuta ya
kula kidogo juu ya kifungashio na funga weka lebo
8.
Peleka sokoni
N:B:
Mafuta
ya kula unayotumia ni lazima yawe yamechemshwa na kupoa
Kwa
maswali, maoni au ushauri juu ya utengenezaji wa Mango pickle wasiliana na mwandishi
wa makala hii kwa simu namba 0758 216548, 0713 330280 au